Salama Na ANNA TIBAIJUKA SE6 EP58 | LA PROFESSEUR PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

YahStoneTown
YahStoneTown
42.8 هزار بار بازدید - 2 سال پیش - #SalamaNa
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460 Nilipoandikiwa ujumbe mfupi na Edwin Bruno ambaye ni mkwe wa Professor kwamba Mama amekubalia kufanya kipindi na sisi siku hiyo ya Jumapili akishatoka church nilihisi kama naota. Mwenyezi Mungu anajua kwa kiasi gani tumekua tukitaka kufanya maongezi nae kwenye kipindi chetu. U busy wake na pengine mara nyingi kutokuwepo Dar es Salaam napo palikua panaleta ugumu, nyengine ilkua ni tarehe zetu za kufanya production na availability yake zilikua zinapishana sana. So unaweza ukaelewa excitement ambayo nilikua nayo baada ya finally samaki kujaa kwenye ndoana. Professor Anna Tibaijuka ni LEGEND miongoni ma magwiji kwenye nchi hii kwa kazi yake na usomi wake na uzazi wake na kujibeba kwake. Kazi mbali mbali ambazo amewahi kuzifanya na kuliwakilisha Taifa hili zinajizungumza kwa sauti kubwa. Ila Safari yake mpaka anafikia kwenda kufanya kazi kwenye Taasisi kubwa duniani hakukumdondokea tu miguuni. Usomi wake ambao aliupambania toka akiwa mdogo na kupata ushirikiano kutoka kwa Marehemu Baba yake ndo kila kitu. Enzi ambazo mtoto wa kike alikua anaandaliwa kuwa Mama wa nyumbani, Baba yake aliamini zaidi kwenye kumpeleka mtoto wake shuleni na kwa mujibu wa Mama Tibaijuka Baba yake alikua aliwasisitiza wazee wenzake kufanya hivyo maana dunia ndo ilikua inaelekea huko, kuna ambao walimsikiliza na wengine ambao waliona anapoteza tu pesa na muda. Mama Tibaijuka na Mimi tuliongelea kuhusu gharama za elimu enzi hizo Mimi nikidhani elimu “ilikua bure” pasi na kujua elimu kipindi hiko ilikua ghali pengine kuliko sasa na ukichukulia shule zenyewe zilikua mbali kweli kweli. Ananiambia pia suala la yeye kutaka kutomuangusha Baba yake ambaye baadhi ya watu walikua wanamcheka kwa kumpeleka Anna shuleni na kuingia gharama zote hizo. Pia ananiambia kuhusu Mama yake kufanya kazi zaidi ili masuala ya nyumbani aweze kuyafanya yeye ili kumsaidia mumewe ambaye pesa yake karibia yote alikua akilipia elimu ya Binti yake. Mama Anna pia ananisimulia humu jinsi ambavyo aliposwa alipokua kidato cha tano na mchumba ilibidi amsubiri mpaka alipomaliza Chuo Kikuu. Nili enjoy kila sekunde ya maongezi haya ambayo kwa kiasi kikubwa naamini yatakua na faida kwetu sote. Ananihadithia pia jinsi ambavyo alienda Sweden na mumewe ambayo alikua huko kikazi na jinsi ambavyo alipata nafasi ya kusoma Chuo Kikuu BURE na ni nafasi ambayo aliipokea kwa mikono miwili na kuhakikisha hafanyi makosa. Mama Anna ameshaifanyia Dunia hii mambo tele ya kimaendeleo wakati akifanya kazi zake UN na baada ya hapo alirudi nyumbani na kukifanya kazi Chama cha Mapinduzi kama Mbunge wa Muleba Kusini na Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo ya makazi. Hapo kwenye uwaziri sasa… Kulikua na mengi yaliyotokea wakati yeye yuko kwenye cheo hiko na ambayo kwa ki ufupi tu tuliyajadili kwenye meza yetu. Mama Anna yuko na Respect ya hali ya juu kwa Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye kwa kiasi kikubwa alimfanya Professor Tibaijuka arudi nyumbani na kulifaidisha Taifa na yale alojifunza wakati anafanya kazi huko kwenye Umoja wa Mataifa. Yangu matumaini utaokota kadhaa kwenye maongezi yetu haya na kwa kiasi flani yatakusaidia kwenye maisha yako. Tafadhali enjoy pia. Love, Salama. Support us through anchor.fm/yahstonetown/support SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs Listen our Podcast on Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬ ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬ GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack ‪YouTube Link bit.ly/YoutubeSalamaNa Soundtrack Yeah by @MarcoChali    • Marco Chali Feat One The Incredible &...   Follow: Twitter: twitter.com/YahStoneTown Instagram: Instagram.com/YahStoneTown Facebook: facebook.com/YahStoneTown Channel Administered by Slide Digital Instagram: www.instagram.com/slidedigitaltz
2 سال پیش در تاریخ 1401/12/22 منتشر شده است.
42,802 بـار بازدید شده
... بیشتر